19 May 2013


Mjumbe wa Mfuko wa Maendeleo ya Kata ya Nyamuswa, wilayani Bunda, Mkoa wa Mara, Bw. Magira Magoma akizungumza, Dar es Salaam juzi jinsi umoja huo ulivyohamasika kutafuta misaada kwa ajili ya maendeleo ya kata hiyo, wakati wa mkutano na wadau wa kata hiyo uliohudhuriwa na Jaji Joseph Warioba (hayupo pichani). Kushoto ni Mjumbe wa mfuko huo, Brigedia Jenerali Ryakitimbo Ryakitimbo wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ).Na Mpiga Picha Wetu

Ngumi Ridhaa Mwanza watimuana

Na Daud Magesa, Mwanza


 CHAMA cha Ngumi za Ridhaa Mkoa wa Mwanza (MBA) kimekumbwa na mgogoro baada ya Katibu Mkuu,Meja Mstaafu Michael Changarawe, kumsimamisha Mwenyekiti wa muda, Kapteni mstaafu,Annasery Mkiwa.
Mgogoro huo wa kutimuana umekuja siku chache baada ya Kapteni Mkiwa, kuwafukuza Meja Changarawe na mchumi mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Madeleke,akiwatuhumu kuchakachua bajeti ya kufanikisha mashindano ya Majiji kutoka sh.milioni 33 hadi sh.milioni 62.
Katibu huyo kwenye barua yake ya kumsimamisha uongozi mwenyekiti huyo wa muda yenye Kumb.Na.MBA/ADM/VOL.-2/14/15 anaeleza kuwa,wamemsimamisha baada ya

TBC kukagua mabati,vifaa vya maji

Na Grace Ndossa


 SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS)limesema kuwa kwa sasa wanahamia kukagua mabati na vifaa vya maji kutokana na kukithiri kwa bidhaa zisizo na viwango hapa nchini.
Kauli hiyo ilitolewa Dar es Salaam jana na Mkurugenzi Mkuu Bw. Joseph Masikitiko wakati walipokutana na wafanyabiashara wa nondo pamoja na wamiliki wa viwanda hivyo kwa ajili ya kuwapatia elimu kuhusu namna ya kuzalisha bidhaa zenye ubora na kupunguza bidhaa hafifu.
Alisema kuwa hii ni kutokana na wafanyabiashara wengi kuzalisha bidhaa zisizo na vuwango na kuchanganya na zenye viwango kwa kuwauzia wateja.
Bw.Masikitiko alisema kuwa ukaguzi huo ni endelevu watakagua kila kiwanda kuhakikisha inapunguza bidhaa hafifu hapa nchini.
Alisema wafanyabiashara pamoja na wamiliki wa viwanda kutoka Dar es Salaam na

Viongozi wa kijiji wanao chochea chuki, mauaji kukamatwa

Na Sammy Kisika, Sumbawanga


 SERIKALI wilayani Sumbawanga imeweka mikakati ya kuanza kuwachukulia hatua kali za kisheria kwa kuwakamata viongozi wa vijiji wote ambao wamekuwa wakishiriki katika kuchochea chuki na kushiriki katika vitendo vya mauaji yanayotokana na imani za kishirikina.
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa wilaya ya Sumbawanga Mathew Sadoyeka katika ziara yake anayoendelea kuifanya kwenye vijiji na kata mbalimbali wilayani humo kwa lengo la kuhamasisha shughuli mbalimbali za maendeleo.
Akizungumza na wananchi wa kata ya Msandamuungano jana, Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa vitendo vya mauaji ya imani za kishirikina vimekuwa vikiongezeka wilayani humo katika

Kada CCM: Bunge linamuaibisha Rais kikwete

Na Suleiman Abeid, Shinyanga


 KADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), mkoani Shinyanga, Mberito Magova, ameliponda Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kudai linastahili kuvunjwa, kuitisha uchaguzi upya kwa sababu linamuaibisha Rais Jakaya Kikwete.
Alionesha kukerwa na kitendo cha Serikali ya CCM kutumia takwimu zisizo sahihi kuonesha uchumi unakua wakati unaporomoka kwa kasi ya kutisha.
Magova ambaye hivi karibuni alistaafu katika nafasi ya Katibu wa CCM Wilaya, aliyasema hayo juzi mjini humo alipokuwa akizungumza na gazeti hili juu ya mustakabali wa Taifa kwa sasa na kudai kuwa, wabunge wameshindwa kuisimamia Serikali badala yake wanatanguliza itikadi za vyama.
Alisema matukio yanayotokea ndani ya Bunge kwa sasa, inaonesha ni jinsi gani wabunge

DC Ludewa aapa kutowasaidia wananchi watakaokumbwa na njaa


Na Nickson Mahundi, Ludewa
MKUU wa wilaya ya Ludewa, Bw.Juma Madaha ameapa kutowasaidia wananchi wilayani humo watakaokumbwa na balaa la njaa kutokana na wananchi hao kuanza kuvuna mahindi na kuyauza kwa bei rahisi na kusahau kuacha akiba ya baadaye.
Bw.Madaha alisema takwimu inaonesha kuwa mtu mzima moja ndani ya mwaka anatumia gunia tano za mahindi kwa chakula lakini baadhi ya wananchi huyauza mahindi yote kutokana na uroho wa fedha hali ambayo husababisha familia kuhangaika zinapokosa chakula na kuilaumu Serikali.
Alisema wilaya ya Ludewa kwa mwaka 2013 imeweza kupata mvua za kutosha kutokana na hali hiyo hakuna kijiji wala kata ambacho kina upungufu wa chakula itashangaza kama kuna familia zimeanza

18 May 2013


Mchuuzi wa bidhaa ndogondogo mwenye mkokoteni akisaka wateja, kama alivyokutwa Barabara ya
Uhuru, Dar es Salaam jana. Matumizi ya mikokoteni katika biashara yanapunguza msongamano wa
vibanda vya biashara mitaani. Picha na Heri Shaaban

Mkazi wa jiji akitupa takataka kwenye Barabara ya Morogoro, kama alivyokutwa Magomeni Kagera Dar
es Salaam jana. Barabara hiyo inaendelea kujengwa na Ksampuni ya STRABAG ya Ujerumani, kama
alivyokutwa jana. Tabia hii inachangia mlipuko wa magonjwa. Picha na Charles Lucas

Twisheni shuleni sasa basi


Na Andrew Ignas


 OFISA elimu wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kwa elimu ya msingi, Bi Elizabeth Thomas amesema serikali hairuhusu masomo ya ziada (twisheni) shuleni kwa kuwa inazorotesha elimu nchini.
Hayo ameyasema jana,wakati wa kongamano la walimu wakuu,waratibu pamoja na wadau mbalimbali wa elimu lililofanyika katika ukumbi wa shule ya msingi ya Mnazi Mmoja ambalo limeshirikisha zaidi wa wajumbe 95 wa halmashauri ya manispaa hiyo.
Akizugungumza na washiriki wa kongamano hilo, Ofisa elimu huyo alisema kuwa serikali inakemea masomo ya ziada (twisheni) kwa kuwa ni njia ambazo walimu wanajikusanyia mapato na si kukuza elimu.
"Kutokana na utafiti uliofanywa tumegundua kwamba walimu wanafanya uzembe kufundisha darasani ili wawashawishi wazazi wa wanafunzi kutenga muda wa masomo ya ziada,"alisema
Waka t i huo huo , Ofisa TAKUKURU wa Mkoa wa Ilala,

Mungu atunusuru yasitokee mabomu mengine-Mama Pinda




 MKE wa Waziri Mkuu Mama Tunu Pinda amesema Watanzania wote kwa pamoja wana kila sababu ya kujinyenyekeza mbele za Mungu na kuendelea kuomba ili pasitokee tena ulipuaji wa mabomu kama lile la Arusha.
Ametoa wito huo jana wakati alipokuwa akizungumza na Katibu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Arusha, Padre Prosper Lyimo wakati alipokwenda kwenye nyumba ya Askofu ili kuwapa pole kwa maafa yaliyowapata waumini wa Parokia teule ya Olasiti jijini Arusha, Mei 5 mwaka huu.
Padre Lyimo alimpokea Mama Pinda kwa niaba ya Askofu Mkuu wa jimbo hilo, Mhashamu Josephat Lebulu ambaye alikuwa safarini kikazi akitoa huduma kwa waumini wengine.
Mama Pinda alisema alilazimika kufika kuwapa pole kwa vile alikuwa amewasili mkoani Arusha kwa shughuli ya kikazi. "Wote tumepokea kwa mshtuko taarifa za ulipuliwaji wa bomu pale Olasiti kwa sababu Watanzania hatujazoea mambo ya mabomu. Tunapaswa wote kwa umoja wetu