RAIS wa
Marekani, Bw. Barack Obama, atakuwa na ujumbe wa watu 700 katika ziara yake ya
siku mbili nchini Tanzania kuanzia Julai Mosi mwaka huu.
Waziri wa Mambo
ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Bernard Membe, aliyasema hayo Dar es
Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari.
Alisema
kutokana na ziara ya kiongozi huyo, alitoa wito kwa wafanyabiashara wenye
hoteli, migahawa, magari ya kukodisha waziboreshe biashara zao ili Wizara hiyo iingie
mkataba nao.
Aliongeza kuwa, akiwa nchini, Bw.
Obama atafanya mkutano na viongozi wa nchi zinazoendelea kwa kuzungumzia
umuhimu wa sayansi na teknolojia katika nchi zao.
“Ugeni huo ni mkubwa, ujio wa
kiongozi huyu utaisaidia nchi kupata pesa