19 May 2013
Ngumi Ridhaa Mwanza watimuana
Na Daud Magesa, Mwanza
CHAMA
cha Ngumi za Ridhaa Mkoa wa Mwanza (MBA) kimekumbwa na mgogoro baada ya Katibu
Mkuu,Meja Mstaafu Michael Changarawe, kumsimamisha Mwenyekiti wa muda, Kapteni
mstaafu,Annasery Mkiwa.
Mgogoro
huo wa kutimuana umekuja siku chache baada ya Kapteni Mkiwa, kuwafukuza Meja
Changarawe na mchumi mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Madeleke,akiwatuhumu
kuchakachua bajeti ya kufanikisha mashindano ya Majiji kutoka sh.milioni 33
hadi sh.milioni 62.
Katibu
huyo kwenye barua yake ya kumsimamisha uongozi mwenyekiti huyo wa muda yenye
Kumb.Na.MBA/ADM/VOL.-2/14/15 anaeleza kuwa,wamemsimamisha baada ya
TBC kukagua mabati,vifaa vya maji
Na Grace Ndossa
SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS)limesema kuwa kwa
sasa wanahamia kukagua mabati na vifaa vya maji kutokana na kukithiri kwa
bidhaa zisizo na viwango hapa nchini.
Kauli hiyo ilitolewa Dar es Salaam
jana na Mkurugenzi Mkuu Bw. Joseph Masikitiko wakati walipokutana na
wafanyabiashara wa nondo pamoja na wamiliki wa viwanda hivyo kwa ajili ya
kuwapatia elimu kuhusu namna ya kuzalisha bidhaa zenye ubora na kupunguza
bidhaa hafifu.
Alisema kuwa hii ni kutokana na
wafanyabiashara wengi kuzalisha bidhaa zisizo na vuwango na kuchanganya na
zenye viwango kwa kuwauzia wateja.
Bw.Masikitiko alisema kuwa ukaguzi
huo ni endelevu watakagua kila kiwanda kuhakikisha inapunguza bidhaa hafifu
hapa nchini.
Alisema wafanyabiashara pamoja na
wamiliki wa viwanda kutoka Dar es Salaam na
Viongozi wa kijiji wanao chochea chuki, mauaji kukamatwa
Na Sammy Kisika, Sumbawanga
SERIKALI
wilayani Sumbawanga imeweka mikakati ya kuanza kuwachukulia hatua kali za
kisheria kwa kuwakamata viongozi wa vijiji wote ambao wamekuwa wakishiriki
katika kuchochea chuki na kushiriki katika vitendo vya mauaji yanayotokana na
imani za kishirikina.
Kauli
hiyo imetolewa na Mkuu wa wilaya ya Sumbawanga Mathew Sadoyeka katika ziara
yake anayoendelea kuifanya kwenye vijiji na kata mbalimbali wilayani humo kwa
lengo la kuhamasisha shughuli mbalimbali za maendeleo.
Akizungumza
na wananchi wa kata ya Msandamuungano jana, Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa
vitendo vya mauaji ya imani za kishirikina vimekuwa vikiongezeka wilayani humo
katika
Kada CCM: Bunge linamuaibisha Rais kikwete
Na Suleiman Abeid, Shinyanga
KADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), mkoani Shinyanga, Mberito Magova,
ameliponda Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kudai linastahili
kuvunjwa, kuitisha uchaguzi upya kwa sababu linamuaibisha Rais Jakaya Kikwete.
Alionesha
kukerwa na kitendo cha Serikali ya CCM kutumia takwimu zisizo sahihi kuonesha
uchumi unakua wakati unaporomoka kwa kasi ya kutisha.
Magova ambaye
hivi karibuni alistaafu katika nafasi ya Katibu wa CCM Wilaya, aliyasema hayo
juzi mjini humo alipokuwa akizungumza na gazeti hili juu ya mustakabali wa
Taifa kwa sasa na kudai kuwa, wabunge wameshindwa kuisimamia Serikali badala
yake wanatanguliza itikadi za vyama.
Alisema matukio
yanayotokea ndani ya Bunge kwa sasa, inaonesha ni jinsi gani wabunge
DC Ludewa aapa kutowasaidia wananchi watakaokumbwa na njaa
Na Nickson Mahundi, Ludewa
MKUU wa wilaya ya Ludewa, Bw.Juma Madaha ameapa kutowasaidia wananchi wilayani humo watakaokumbwa na balaa la njaa kutokana na wananchi hao kuanza kuvuna mahindi na kuyauza kwa bei rahisi na kusahau kuacha akiba ya baadaye.
Bw.Madaha alisema takwimu inaonesha kuwa mtu mzima moja ndani ya mwaka anatumia gunia tano za mahindi kwa chakula lakini baadhi ya wananchi huyauza mahindi yote kutokana na uroho wa fedha hali ambayo husababisha familia kuhangaika zinapokosa chakula na kuilaumu Serikali.
Alisema wilaya ya Ludewa kwa mwaka 2013 imeweza kupata mvua za kutosha kutokana na hali hiyo hakuna kijiji wala kata ambacho kina upungufu wa chakula itashangaza kama kuna familia zimeanza
18 May 2013
Twisheni shuleni sasa basi
Na Andrew Ignas
OFISA elimu wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kwa elimu ya msingi, Bi Elizabeth Thomas amesema serikali hairuhusu masomo ya ziada (twisheni) shuleni kwa kuwa inazorotesha elimu nchini.
Hayo ameyasema jana,wakati wa kongamano la walimu wakuu,waratibu pamoja na wadau mbalimbali wa elimu lililofanyika katika ukumbi wa shule ya msingi ya Mnazi Mmoja ambalo limeshirikisha zaidi wa wajumbe 95 wa halmashauri ya manispaa hiyo.
Akizugungumza na washiriki wa kongamano hilo, Ofisa elimu huyo alisema kuwa serikali inakemea masomo ya ziada (twisheni) kwa kuwa ni njia ambazo walimu wanajikusanyia mapato na si kukuza elimu.
"Kutokana na utafiti uliofanywa tumegundua kwamba walimu wanafanya uzembe kufundisha darasani ili wawashawishi wazazi wa wanafunzi kutenga muda wa masomo ya ziada,"alisema
Waka t i huo huo , Ofisa TAKUKURU wa Mkoa wa Ilala,
Mungu atunusuru yasitokee mabomu mengine-Mama Pinda
MKE wa Waziri Mkuu Mama Tunu Pinda amesema Watanzania wote kwa pamoja wana kila sababu ya kujinyenyekeza mbele za Mungu na kuendelea kuomba ili pasitokee tena ulipuaji wa mabomu kama lile la Arusha.
Ametoa wito huo jana wakati alipokuwa akizungumza na Katibu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Arusha, Padre Prosper Lyimo wakati alipokwenda kwenye nyumba ya Askofu ili kuwapa pole kwa maafa yaliyowapata waumini wa Parokia teule ya Olasiti jijini Arusha, Mei 5 mwaka huu.
Padre Lyimo alimpokea Mama Pinda kwa niaba ya Askofu Mkuu wa jimbo hilo, Mhashamu Josephat Lebulu ambaye alikuwa safarini kikazi akitoa huduma kwa waumini wengine.
Mama Pinda alisema alilazimika kufika kuwapa pole kwa vile alikuwa amewasili mkoani Arusha kwa shughuli ya kikazi. "Wote tumepokea kwa mshtuko taarifa za ulipuliwaji wa bomu pale Olasiti kwa sababu Watanzania hatujazoea mambo ya mabomu. Tunapaswa wote kwa umoja wetu
Subscribe to:
Posts (Atom)