06 February 2012

Uchambuzi wa vitabu:

Kidato cha 3 & 4
Vitabu vinavyoichambua jamii na matatizo yake.

Vitabu :  Watoto wa Maman’tilie na Joka la Mdimu
Mpitiaji:   Shabani Njenge 0718868298

KATIKA uhakiki huu tutaangalia namna vitabu hivi viwili:  Watoto wa Maman’tilie na Joka la Mdimu vinavyofanana na kutofautiana.

Ipo  tofauti baina ya vitabu hivi viwili, tofauti hiyo inajitokeza  katika mambo mbalimbali  yakiwemo haya:

Dhamira kuu.
Dhamira Kuu  inayojitokeza katika  Riwaya ya Watoto wa Maman’tilie ni kuzungumzia juu  ya watoto wa mitaani  na hatima yao.  Riwaya  inaonesha  namna  watoto  wanavyo poteza mwelekeo wa maisha pindi waachapo kusoma.

Zita Peter Musa Kurwa na Doto wametumiwa na mwandishi kuonyesha  ukweli  wa jambo hilo. Watoto hao baada ya kushindwa kuendelea na shule waliingia  mitaani na hatimaye kujihusisha  na vitendo viovu vikiwemo uuzaji wa dawa za kulevya  na wizi.

Riwaya ya Joka la Mdimu  kwa upande inazungumzia  kuhusu ufisadi. Mwandishi  kwa kutumia mbinu za Kifasihi anaelezea  kuhusu wizi wa fedha za kigeni uliofanyika  katika  benki kuu na hivyo kusababisha  serikali kukosa fedha za kununulia mafuta kutoka nje hali iliyosababisha nchi kukumbwa na hali ngumu kiuchumi.

 “Hebu angalia hili tatizo la mafuta. Nasikia meli imekuja na mafuta, benki hakuna hata senti ya fedha za kigeni.  Imegeuza na kurudi na kutuachia madeni ya kusafirisha mafuta hayo pamoja na ushuru wa bandari. Sasa kama usemavyo sukari inapelekwa nje, mbona tunashindwa kulipia mafuta.

Siasa na uongozi wa nchi
Dhamira  nyingine inayoonyesha kutofutiana  kwa vitabu hivi
 ni dhana ya siasa na uongozi wananchi.

Watoto wa Maman’tilie haizungumzi jambo lolote kuhusu wanasiasa wetu, badala yake inaelekeza  mjadala wake kwenye dhana  ya uongozi wa kifamilia 

Kuhusiana na suala zima  la uongozi wa familia, riwaya hii imeonyesha  namna wazazi wanavyotakiwa kuwa viongozi wazuri wa familia  kwa kuwapa watoto malezi yanayowafanya kuwa na uwezo wa kuendesha maisha yao wao wenyewe hapo baadaye. 

Jambo hili tunaweza kuliona kupitia malezi ambayo mamantilie anawapa watoto wake.Mama huyo anawashirikisha Zita na Peter kwenye shughuli  yake ya kupika na kuuza chakula. Na tunawaona Zita na Peter wakiyamdu maisha pale wanapobaki peke yao  wakati  Maman’tilie anaposafiri  kwenda Matombo, Morogoro.

Riwaya ya Joka la Mdimu tofauti na Riwaya ya Watoto wa Maman’tilie yenyewe imezungumzia kuhusu uongozi wa kitaifa.
Mwandishi anaelezea namna uongozi wa nchi ulivyo kiini cha  matatizo ya kimaisha yanayowakabili  wananchi walio wengi


Nafasi ya mwanamke katika jamii.
Tofauti kati ya Watoto wa Maman’tilie na Joka la Mdimu imejitokeza pia katika kipengele cha nafasi ya mwanamke.

Riwaya ya Watoto wa Maman’tilie kwa kiasi kikubwa inamwonyesha mwanamke kama  mzalishaji mali
Nafasi hiyo inajibainisha kupitia mhusika Maman’tilie kutokana na namna alivyokuwa akijishughulisha na kazi ya kupika na kuuza chakula.

Nafasi  kama hiyo kwa kweli hatuioni  katika Joka la Mdimu  kwa kiwango kinachoweza kulinganishwa na hicho kionekanacho katika Watoto wa Maman’tilie.

Joka la Mdimu kwa upande wake inamwonesha mwanamke kama chombo cha starehe. Nafasi hii inajibainisha kutokana na namna Brown kwacha alivyokuwa akiwatumia wanawake mbalimbali kujistarehesha.

Athari za maendeleo ya sayansi na tekinolojia
Watoto wa Maman’tilie  imeonyesha namna uvumbuzi wa video
ulivyoharibu vijana wetu.  Vijana wetu  kutokana na kuangalia picha za video zikiwemo zile zinazohusu ujambazi hatimaye nao pia huiga ujambazi huo na kutenda.

Riwaya hii inathibitisha ukweli huo kutokana na namna  inavyoelezea kuhusu jinsi Dan na wenzake walivyopanga kwenda kuiba kwa Rhemtulah kwa kutumia mbinu za ujambazi ambazo walikuwa wakiziona katika picha  za video.

Lazima mambo yaende  kimafia Dan alikuwa kaathirika sana na
Video za ujambazi wa ulaya (uk.41)
Dhamira kama hii hatuioni katika Joka la mdimu

Tatizo la imani za ushirikina
Dhamira hii amejitokeza katika Joka la Mdimu. Mtunzi anatueleza namna imani za ushirikina zilivyoenea katika jamii
Kiasi cha kutumiwa hata katika shughuli za michezo.

Jambo hilo linaonyeshwa na mtunzi pale anapoelezea  kuhusu mechi kati ya timu mbili tofauti za mpira; timu ya City Devils  na Sega Warriors (uk. 58-59)  Dhamira hii haikujitokeza katika Watoto wa Mamantilie.

Tofauti kati ya Joka la Mdimu na Watoto  wa Maman’tilie inajitokeza na katika fani pia; katika vipengele tofauti vikiwemo hivi: 
Wahusika:
Joka la Mdimu inatumia wahusika wa kawaida na wahusika vielelezo. Hawa ni wahusika ambao hupewa majina kulingana 
na aidha tabia zao au umbile lao, kazi zao n.k.

Wahusika  hao  ni Brown kwacha na Dakta Mikwala.  Brown Kwacha  ni mtu  apendaye pesa na Dakta Mikwala pia ni mtu apendaye rushwa ingawaje  mwanzoni   huwapiga mkwara   watu  ili  kutaka kuonyesha kuwa yeye si mla rushwa

Mandhari.
Joka la Mdimu mandhari yake haitajwi wazi, Watoto wa Maman’tilie Madhari yake  imetajwa  wazi kuwa ni Dar es salam na vitongozi vyake:  ambavyo ni Kisutu, Manzese  na Tabata.

Jina  la kitabu
Tofauti kati ya vitabu hivi imejitokeza pia kwenye kiini cha majina. Jina la Joka la Mdimu  limetokana na dhana ya Uongozi. Mwandishi anawalinganisha viongozi wasiofaa na nyoka wa kijani  aishiye katika mdimu ambapo unaweza ukadhani ni mdimu kumbe ni nyoka.

Na viongozi pia baadhi yao kwa mtazamo wa kawaida huonekana kama wapo upande wa wananchi kumbe ni wasaliti.

Jina la  Watoto wa  Maman’tilie  limetokana na mhusika mkuu Maman’tilie.

Pamoja na tofauti hizo, vitabu hivi  vina hali ya kufanana  kimaudhui.  Hii ni kutokana na kuwepo kwa hali ya mwingiliano katika baadhi ya  dhamira. Kwa mfano :

Itaendelea...

No comments:

Post a Comment